Home Uncategorized DILUNGA ATAJA SABABU YA KUTUSUA SIMBA

DILUNGA ATAJA SABABU YA KUTUSUA SIMBA

HASSAN Dilunga, kiungo mshambuliaji wa Simba amesema kuwa kikubwa ambacho kinambeba ndani ya klabu hiyo nikujituma na kufanya kazi bila kuchoka.

Kabla ya Ligi Kuu Bara kusimamishwa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona, Dilunga alikuwa ametupia mabao sita ndani ya Simba ambayo imefunga mabao 63.

Dilunga amesema:”Kikubwa ilikuwa ni kutazama namna gani ninaweza kuipa matokeo timu yetu ya Simba ambayo ina malengo ya kufika hatua za kimataifa.

“Ushirikiano mkubwa ndani ya Simba ikiwa ni pamoja na sapoti ya wachezaji wenzangu pamoja na uongozi ni jambo ambalo linachangia kwenye mafanikio ndani ya Simba,” .

Mabingwa hao watetezi wanaongoza ligi wakiwa nafasi ya kwanza na pointi zao kibindoni ni 71.

SOMA NA HII  YANGA YAWEKEZA NGUVU ZOTE HUKU BAADA YA KUPOTEZA LIGI KUU BARA NA FA