Home Uncategorized HAWA HAPA WANAOMBEBA FEI TOTO YANGA

HAWA HAPA WANAOMBEBA FEI TOTO YANGA

FEISAL Salum, kiungo wa Yanga amesema kuwa uwepo wa Haruna Niyonzima na Papy Tshishimbi umekuwa ukimfanya kuwa Bora.

Kabla ya Ligi Kuu Bara kusimamishwa ili kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona Fei alikuwa kwenye ubora wake na kwenye mechi dhidi ya Simba Machi 8 Uwanja wa Taifa alitibua mipango ya wapinzani wake.


Mchezo huo Yanga ilishinda bao 1-0 na kuwafanya wasepe na pointi tatu jumlajumla.

Fei amesema:-“Kikubwa ni suala la nidhamu pia kocha alikuwa anaelewa kile ninachokifanya kwani mwanzo alikuwa haelewi kile ninachokifanya.


 “Mpira siyo kitu cha kucheza mtu mmoja pekee Ila uwepo wa Haruna Niyonzima na Papy Tshishimbi ulikuwa unanibeba,” alisema.

SOMA NA HII  STRAIKA MGHANA YANGA AIBUKA NA MPYA