Home Uncategorized TOTTHENHAM, JUVENTUS USO KWA USO KWA KIUNGO WA CHELSEA

TOTTHENHAM, JUVENTUS USO KWA USO KWA KIUNGO WA CHELSEA


WILLIAN nyota anayekipiga ndani ya Chelsea amewekwa kwenye rada za Juventus na Tottenham ambazo zimetajwa kumuwinda kiungo huyo.

Willian alikuwa akihusishwa kutimka ndani ya Klabu ya Chelsea katika usajili uliopita lakini sasa Juventus wanaonekana kushikilia bango la kutaka kumsajili.

Imeelezwa kuwa nyota huyo anataka kusalia ndani ya London hivyo huenda Spurs wakaipata saini yake.


Kiungo huyo mpaka sasa hana uhakika wa kubaki ndani ya Chelsea baada ya kuambiwa aongeze mkataba wa mwaka mmoja huku yeye hesabu zake zikiwa ni kusaini kandarasi ya miaka miwili.

SOMA NA HII  AZAM FC WAANZA KWA USHINDI KAGAME