Home Uncategorized KOCHA LIGI KUU BARA AKUBALI UWEZO WA KAGERE

KOCHA LIGI KUU BARA AKUBALI UWEZO WA KAGERE



HITIMANA Thiery, Kocha Mkuu wa Namungo amesema kuwa miongoni mwa washambuliaji walio hatari ndani ya Ligi Kuu Bara ni pamoja na Meddie Kagere.


Akizungumza na Saleh Jembe, Hitimana amesema kuwa amekuwa akiwatazama washambuliaji wengi uwanjani ambao ni hatari ambapo na Kagere ni miongoni mwao.

“Nimekuwa nikitazama washambuliaji wengi ambao ni hatari ndani ya ligi jina la Kagere ni miongioni mwao.

“Amekuwa na mwendelezo mzuri na wastani wa kufunga mabao ndani ya mechi ambazo anacheza ambapo ukitazama kwa sasa ana mabao zaidi ya 10 si wa kubeza,” amesema.

Kagere amehusika kwenye jumla ya mabao 19 yaliyofungwa na Simba msimu huu ambayo imefunga mabao 63.
SOMA NA HII  KOSI HILI LA MASTAA KARANTINI INAWAHUSU