Home Uncategorized MOLINGA APANIA KUFUNGA MABAO MENGI KWENYE LIKI

MOLINGA APANIA KUFUNGA MABAO MENGI KWENYE LIKI

DAVID Molinga, mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa anataka kufunga mabao mengi zaidi pale Ligi Kuu Bara itakaporudi.

Molinga ametupia mabao nane ndani ya ligi akiwa ni kinara kwa Yanga ambayo imefunga mabao 31 kwenye mechi 27.

Molinga amesema:”Ikiwa nitapata nafasi zaidi ya kuanza kikosi cha kwanza pale ligi ikirudi nina amini nitafunga mabao mengi zaidi ya haya nane niliyonayo kwa sasa na yote yatawezekana kwani ninafanya mazoezi ,” .

Ligi Kuu Tanzania Bara ilisimamishwa Machi 17 na Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa baada ya kupatikana mgonjwa wa kwanza nchini.

SOMA NA HII  HAKUNA SILLAH WALA ONANA MWAMBA HUYU HAPA