MOHAMED Rashid, nyota wa JKT Tanzania anayekipiga kwa mkopo akitokea Simba amesema kuwa kuna umuhimu wa kila mmoja kuchukua tahadhari ya kujilinda dhidi ya Virusi vya Corona ili kubaki salama.
Akizungumza na Saleh Jembe, Rashid amesema kuwa amekuwa akitumia muda mwingi nyumbani kutokana na kushindwa kuendelea na mazoezi ikiwa ni njia ya kujilinda na Corona.
“Muda mwingi natumia nikiwa nyumbani kwa sasa tofauti na wakati ule kabla ya janga hili kutokea, nimekuwa nikiwasihi na wengine pia kama hawana shughuli ya muhimu itakayowatoa nje wabaki nyumbani.
“Kuna vitu vingi tunakosa kwa sasa lakini hakuna namna ni lazima tuombe hili janga lipite na kila mmoja achukue tahadhari,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.