Home Uncategorized MPANGO MKUBWA WA KUMALIZA LIGI KUU ENGLAND NI KESHO

MPANGO MKUBWA WA KUMALIZA LIGI KUU ENGLAND NI KESHO


KUTOKANA na kusimamishwa kwa ligi mbalimbali duniani kupisha maambukizi ya Virusi vya Corona, viongozi wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu England wanatarajiwa kufanya kikao kesho kujadili hatma ya Ligi hiyo.

Mpango mkubwa uliopo kwa timu hizo ndani ya msimu wa 2019-20 ni kuona kwamba wanamaliza msimu ifikapo 30,Juni 2020.

Mbali na ishu ya kumaliza msimu pia kuna suala la kujadili kuhusu mikataba ya wachezaji ambao inakaribia kumeguka hivi karibuni pamoja na mikataba ya makampuni yalioingia na timu kubwa duniani.

Miongoni mwa klabu ambazo zipo Kwenye mpango wa kubadili jezi zao ni pamoja na Liverpool ambao walikuwa wanatumia nembo ya New Balance na sasa msimu ujao wanahitaji kutumia nembo ya Nike huku Klabu za Watford na Newcastle zikiwa kwenye mpango wa kubadili wasambazaji wao wa vifaa.

SOMA NA HII  SIMBA:MASHABIKI TUPENI SAPOTI TUTAENDELEA PALE TULIPOISHIA