Home Uncategorized MSHAMBULIAJI AZAM FC AZIDI KUJINOA AKIWA NYUMBANI

MSHAMBULIAJI AZAM FC AZIDI KUJINOA AKIWA NYUMBANI

MBARAKA Yusuph, mshambuliaji wa Azam FC amesema kuwa kwa sasa anaendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona huku akifanya mazoezi binafsi akiwa nyumbani.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mbaraka amesema kuwa amekuwa akichukua tahadhari  kulinda afya yake pamoja na wale wanaomzunguka.

“Nipo makini kwa sasa nikichukua tahadhari wakati huu wa maambukizi ya Virusi vya Corona na ninafanya mazoezi ili kuendelea kuwa bora.

“Nina amini wakati ukifika kila kitu kitakuwa sawa na tutarejea kwenye maisha yetu ya kawaida jambo la msingi ni kuchukua tahadhari ili kuwa salama,” amesema. 

SOMA NA HII  KASI YA NYOTA MPYA WA SIMBA YAMKOSHA MBELGIJI WA SIMBA, ALICHOKIFANYA DAKIKA 12 NI BALAA