INAELEZWA kuwa Uongozi wa Simba umeamua kumalizana na mchezaji wao Deo Kanda ambaye alikuwa kwenye hesabu za kutua ndani ya Yanga msimu ujao.
Kanda ambaye alitua Bongo akitokea Congo kwa mkopo wa muda wa mwaka mmoja ambapo msimu ukimeguka naye dili lake lilikuwa linameguka ameongezewa dili jingine.
Habari zinaeleza kuwa kutokana na mchango wake kuwa mkubwa ameongezewa kandarasi ya miaka miwili ili abaki ndani ya Simba.
Mtendaji Mkuu wa Simba, Senzo Mazingisa alipotafutwa azungumzie suala hili hakuwa tayari kuweka wazi.
Kanda amefunga mabao saba ndani ya Simba ambayo imefunga jumla ya mabao 63 kwenye Ligi Kuu Bara.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.