IMEELEZWA kuwa Klabu ya Yanga inaisaka saini ya nyota wa Kariobangi Sharks FC Yidah Sven Yidah ili aongeze nguvu kwenye kikosi hicho.
Nyota huyo ambaye ni kiungo raia wa Kenya anakipiga pia kwenye timu ya Taifa ya chini ya miaka 23.
Uwezo wake wa kukaba na kuzuia mashambulizi ya wapinzani inaelezwa kuwa sababu ya Yanga kuvutiwa naye na ikiwa mambo yatakwenda sawa anaweza kutua bure kwani mkataba wake unameguka mwisho wa msimu huu.
Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonion Nugaz amesema kuwa kwa sasa ni subira inahitajika kwani mpango mkubwa uliopo ni kusuka kikosi kipya.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.