Home Uncategorized BANDA AFUNGUKIA ISHU YA LIGI YA AFRIKA KUSINI KUFUTWA

BANDA AFUNGUKIA ISHU YA LIGI YA AFRIKA KUSINI KUFUTWA

Habari za Yanga SC


ABDI Banda beki kutoka Bongo anayekipiga ndani ya Highlands Park inayoshiriki Ligi Kuu nchini Afrika Kusini amesema kuwa kama ligi yao itafutwa fresh tu hamna noma.

Kwa sasa Ligi Kuu ya Afrika Kusini pamoja na ligi mbalimbali duniani zimesimama kutokana na janga la Virusi vya Corona.


Banda amesema kuwa kwa sasa wameambiwa waendelee kusubiri mpaka Mei 21 kujua maamuzi gani yatachukuliwa.

“Ikitokea ligi imefutwa ni kweli kwa kiasi fulani nitaathirika katika masuala ya takwimu nilizotengeneza msimu huu ila masuala ya afya ni muhimu wakiamua kufuta sawa siwezi kuwapinga,”.

SOMA NA HII  YUSUPH MHILU: TUMEANZA KUJENGA HALI YA KUJIAMINI