Home Uncategorized GWAMBINA FC YAWAOMBA WADHAMINI WAJITOKEZE KUIPA SAPOTI

GWAMBINA FC YAWAOMBA WADHAMINI WAJITOKEZE KUIPA SAPOTI

UONGOZI wa Gwambina FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza umewaomba wadau kujitokeza kwa sasa kuipa sapoti timu hiyo ambayo inaamini mambo yakiwa sawa kwenye upande wa ligi itashiriki Ligi Kuu Bara msimu ujao.

Ofisa Masoko wa Gwambina FC,Mohamed Ngaiza amesema kuwa wanawaomba wadau kujitokeza kwa wingi kuwekeza ndani ya timu hiyo.

“Msimu ujo idara ya masoko tutakuwa na punguzo kubwa la matangazo hivyo ni fursa kwa wafanyabiashara kuja kwa wingi kuwekeza kwetu.

“Tupo vizuri kwenye kutangaza bidhaa na matangazo ya wadhamini wetu kuanzia kwenye jezi mpaka vifaa hivyo ninawaomba wadau na wafanyabiashara wajitokeze kwa wingi,” amesema.

SOMA NA HII  MORRISON ASIMULIA NAMNA ALIVYOFUATWA NA SIMBA KABLA YA MCHEZO WAO MACHI 8