Home Uncategorized NYONI AWAOMBA WATANZANIA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA

NYONI AWAOMBA WATANZANIA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA


ERASTO Nyoni, beki kiraka ndani ya Simba amewaomba watanzania kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.
Akizungumza na Saleh Jembe, Nyoni amesema kuwa janga la Corona lipo na limesimamisha mengi hivyo ni muhimu kila mmoja akachukua tahadhari.
“Muhimu kila mmoja kuongeza umakini katika kuchukua tahadhari dhidi ya Corona, janga hili lipo tusipuuzie.
“Hata mimi pia ninajali na kufuata kanuni za afya ambazo zimewekwa na wizara ya afya pamoja na Serikali ni muhimu kila mmoja kuchukua tahadhari,” amesema Nyoni.
SOMA NA HII  YANGA YAWAITA MASHABIKI UWANJANI