Home Uncategorized THOMAS PARTEY ATAKA KUIBUKIA ARSENAL

THOMAS PARTEY ATAKA KUIBUKIA ARSENAL


THOMAS Partey, kiungo wa Atletico Madrid amesema kuwa anataka kujiunga na Klabu ya Arsenal msimu ujao.

Partey amewekwa kwenye hesabu za Arsenal iliyo chini ya Kocha Mkuu, Mikel Arteta ambaye ameonyesha nia ya kuhitaji saini yake.

Staa huyo raia wa Ghana mkataba wake ndani ya Atletico Madrid unameguka msimu wa 2023 na kiwango chake cha usajili kinatajwa kufikia pauni milioni 45.

Inaelezwa kuwa ili Arsenal wapate saini ya nyota huyo basi inabidi wakubali kumuachia Alexandre Lacazette.

SOMA NA HII  AZAM FC YASHANGAZWA NA MATOKEO MABOVU NDANI YA LIGI