Home Uncategorized SIMBA YATAKA KUBEBA MATAJI MAKUBWA MAWILI

SIMBA YATAKA KUBEBA MATAJI MAKUBWA MAWILI

MTENDAJI Mkuu wa Simba, Senzo Mbatha amesema kuwa mpango mkubwa uliopo kwa timu hiyo ni kupambana kupata mataji makubwa mawili msimu huu wa 2019/20.

Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara leo walikuwa wanazindua mpango kazi wa kusambaza taarifa mtandaoni ambao ni tovuti itakayorahisisha kazi ya kutoa taarifa.

Senzo amesema:”Lazima tujikite kuhakikisha tunashinda ligi kuu na FA. Hiyo ndio dhamira yetu kwa sasa.”

Kombe la FA Simba imetinga robo fainali huku kwa upande wa Ligi Kuu Bara ikiwa nafasi ya kwanza na pointi 71 baada ya kucheza mechi 28.

SOMA NA HII  CHELSEA YAKUBALI KUMUACHIA NYOTA WAO LUZ KWA HASARA KUTUA ARSENAL