PASCAL Wawa beki kisiki wa Simba amesema kuwa hana hesabu za kuleta familia yake Bongo kwa sasa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona.
Machi 17, Ligi Kuu Bara Bara ilisimamishwa na Serikali kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vinaivurugavuruga dunia ila kwa sasa inatarajiwa kurejea Juni Mosi.
Wawa amesema kuwa mambo bado sio shwari haoni haja ya kuleta familia yake ambayo ipo nchini Ivory Coast.
“Tunapita kipindi kigumu kwa sasa ila hakuna chaguo la kufanya ni lazima tuombe dua mambo yawe safi, sina mpango wa kuleta familia Tanzania kwa sasa huko walipo tunawasiliana,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.