UONGOZI wa Namungo FC umesema kuwa iwapo Yanga inahitaji saini ya nyota wao Bigirimana Blaise ni suala la kuzungumza kwani inawezekana.
Imekuwa ikielezwa kuwa Yanga inahitaji kuboresha safu ya ushambuliaji na inahitaji kupata saini ya Blaise anayekipiga Namungo.
Blaise amefunga mabao 10 ndani ya timu hiyo iliyo nafasi ya tano ikiwa imefunga mabao 34 na ina pointi 50 kibindoni.
Ofisa Habari wa Namungo FC, Kidamba Namlia amesema kuwa wamekuwa wakiskia kuwa Blaise anahitajika na Yanga ila halijafika mezani suala hilo.
“Yanga hawajaja mezani na imekuwa ikielezwa kuwa wanahitaji saini ya Blaise kama ni kweli waje mezani tuzungumze,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.