Home Uncategorized HIVI HAPA VIGONGO VITATU VYA AZAM FC JUNI

HIVI HAPA VIGONGO VITATU VYA AZAM FC JUNI


MECHI za Ligi Kuu Tanzania Bara zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi ifikapo Juni 13 baada ya Serikali kuruhusu masuala ya michezo kuendelea pale mambo yalipoishia.

Hakukuwa na mechi ya ushindani tangu Machi 17 kutokana na janga la Virusi vya Corona kwa sasa Serikali imeruhusu masuala ya michezo kwa kueleza kuwa maambukizi yameanza kupungua.

Azam FC iliyo chini ya Arstica Cioaba ipo nafasi ya pili tayari ilishaanza mazoezi tangu Mei 27 kwa mwezi Juni ina vigongo vikali vitatu. 

Hizi hapa za mwezi Juni kwa Azam FC;-Juni 14, Azam  FC v Mbao Uwanja wa Azam Complex.

Juni 21, Yanga v Azam FC Uwanja wa Taifa.

Juni 24, Kagera Sugar v Azam Uwanja wa Kaitaba.

SOMA NA HII  MCHEZAJI SIMBA ATUA LIPULI