KOCHA Mkuu wa KMC, Harerimana Haruna amesema kuwa kichapo cha mabao 3-1 walichopata kutoka kwa Simba sio halali kwa kuwa mabao mawili yaliyofungwa na nahodha John Bocco alikuwa ameotea.
Simba iliwafunga KMC kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Juni 8, Uwanja wa Simba, Mo Arena.
Mabao ya Simba mawili yalifungwa na Bocco huku moja likifungwa na kiungo mshambuliaji wa Simba, Ibarahim Ajibu.
“Tumefungwa bao moja la halali hivyo matokeo yaliyo sahihi ni 1-1, mabao mawili ya Bocco yote aliotea hivyo mimi sijui imekuajekuaje,” amesema.
Bao la KMC lilipachikwa kimiani na Charlse Ilanfya ambaye alikuwa ni mwiba ndani ya Simba.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.