Home Uncategorized SALIBOKO MTUPIAJI NAMBA MBILI WA LIPULI ATAJA ALIPOJICHIMBIA

SALIBOKO MTUPIAJI NAMBA MBILI WA LIPULI ATAJA ALIPOJICHIMBIA


DARUESH Saliboko, mshambuliaji namba mbili wa Klabu ya Lipuli amesema kuwa ataripoti kambini hivi karibuni kwa kuwa kwa sasa kuna mambo anayaweka sawa.

Lipuli iliripoti kambini tangu Mei 31 na tayari walishaanza mazoezi ya kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara chini ya Kocha Mkuu, Nzeyimana Mailo.

Akizungumza na Saleh Jembe, Saliboko amesema kuwa bado hajaripoti kambini kutokana na kushughulikia masuala yake binafsi.

“Bado sijaripoti kambini kwa sasa nipo zangu Morogoro kuna mambo ninayaweka sawa kila kitu kikikamilika nitareja kambini kuungana na wachezaji wenzangu.”

Sabilo kibindoni ametupia mabao nane kati ya mabao 35 yaliyofungwa na Lipuli.

SOMA NA HII  SIMBA KUMVUTA KIPA MRUNDI ILI KUMPA CHANGAMOTO MANULA