Home Uncategorized SIMBA WAICHOKONOA YANGA KIMTINDO HIVI

SIMBA WAICHOKONOA YANGA KIMTINDO HIVI


BAADA ya Uogozi wa Yanga kusema kuwa wachezaji wao watatu wameongezeka uzito, Ofisa Habari wa Simba Haji Manara kama amewajibu kimtindo kwa kuwataja wachezaji wa Simba hali zao.

Ipo hivi Jana, kwenye mazoezi, Kocha Msaidizi wa Yanga, Charles Mkwasa alisema kuwa wachezaji watatu wa Yanga wameongezeka uzito na wamepewa program maalumu kwa ajili ya kupunguza uzito wao.

Manara kupitia Ukurasa wake rasmi wa Instagram ameandika namna hii:”Wachezaji wetu wote wapo sawa, hakuna aliyeongezeka unene kama kiboko wala hakuna aliyeongezeka urefu, John Bocco na wenzie wapo vile vile kwa kuwa walijua kuitunza miili yao.

“Wachezaji wetu hawali Chips Mayai zinazojazwa makachumbari, wanajua lishe ya professional player,”.

SOMA NA HII  KIBU KWA SIMBA ATAKIPIGA SANA MWAMBA HUYU HAPA ATIA NENO