Home Uncategorized TFF YAWEKEZA NGUVU KUBWA KWA VIJANA, SASA KUFUNGUA SHULE ZA VIPAJI MAALUM

TFF YAWEKEZA NGUVU KUBWA KWA VIJANA, SASA KUFUNGUA SHULE ZA VIPAJI MAALUM


MKURUGENZI wa masuala ya Ufundi ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) Oscar Milambo amesema kuwa ni mpango mkubwa uliopo kwa sasa ni kuendeleza vipaji kwa vijana ili waweze kufikia malengo ambayo wamejiwekea.

Milambo amesema kuwa ili kuwa na timu bora kwa taifa ni lazima kuwekeza kwa vijana jambo litakalosaidia kuwa na chaguo la wachezaji wengi.

“Muhimu kuwa na vituo vingi nchini ambavyo vitasaidia kukuza uwezo wao na kuendelea kuwalinda wakati wanaendelea kukua.

“Malengo yetu kwa sasa ni kuona kwamba kwenye kila mkoa kuna kuwa na shule maalum ambazo zitasaidia kuendeleza vipaji vyao na itasaidia kuwa na hazina kubwa kwenye timu ya taifa,” amesema.

SOMA NA HII  UBABE WA YANGA WAIHAMISHA GEITA GOLD