Home Uncategorized AZAM FC WAKUTANA NA RUNGU LA TFF

AZAM FC WAKUTANA NA RUNGU LA TFF


TIMU ya Azam FC imepigwa faini ya shilingi laki tano (500,000) kwa kosa la wachezaji na maofisa wa timu hiyo kuingia uwanjani kwa kupitia lango tofauti na lililoandaliwa.


Taarifa inasema kuwa Azam FC walidai kwamba walizuiwa kuingia kupitia mlango elekezwa katika mechi iliyochezwa Juni 23, 2020 Uwanja wa Karume Mkoani Mara. 

Adhabu hii imetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 14(49) kuhusu taratibu za mchezo.

Mechi hiyo ilikamilika kwa Biashara FC kutoshana nguvu ya kufungana bao 1-1 na Azam FC.

SOMA NA HII  PLAYOFF LIVE: KAGERA SUGAR 0-0 PAMBA