BEKI wa timu ya Yanga, Juma Abdul, amewapongeza Simba kwa kufanikiwa kutetea taji la Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2019/20.
Akizungumza na gazeti la BINGWA jana, Abdul alisema pamoja na Simba kutwaa taji hilo kwa misimu mitatu mfululizo wajui msimu wa 2020/21, hawataweza kutetea tena.
Abdul alisema watahakikisha msimu unaokuja ubingwa wa ligi hiyo, unatua Jangwani baada ya kuukosa kwa miaka mitatu mfululizo.
Hata hivyo, Abdul alisema walichokifanya Simba si jambo geni, kwani waliwahi kutwaa ubingwa mara tatu mfululizo kabla yao.
“Kwa nafasi yangu nawapongeza Simba kwa kuwa mabingwa wa ligi na wamefanya jambo ambalo tulilifanya Yanga miaka mitatu iliyopita,”
“Lakini ubingwa huu usiwape kiburi cha kuona wamemaliza na msimu ujao wataweza kuchukua tena, hicho kitu hakitotokea wajue hili kabisa, tutakuja kivingine na lazima ubingwa tuchukue,” alisema
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.