Home Uncategorized ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA NI MOTO

ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA NI MOTO

DROO ya Hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imewekwa wazi, Barcelona huenda ikavaana na Bayern Munich na Manchester City ikavaana na Juventus.

 Ratiba  hiyo imewekwa wazi huku baadhi ya timu zikiwa na viporo vya hatua ya 16 bora hii ni kutokana na michuano hiyo kusimama kutokana na janga la Virusi vya Corona ambalo liliivurugavuruga dunia.
  Barcelona mchezo wake wa awali ilitoa sare ya 1-1 na Napoli na sasa itacheza Agosti pale Camp Nou  na ikishinda itakutana na Bayern Munich. Man City wao waliifunga  Real Madrid 2-1 pale Santiago Bernabeu na sasa watakuwa Etihad na atakaye shinda kati ya Juventus na Lyon  ambapo Juve alipoteza kwa bao 1-0.
 Klabu ambazo ratiba yao ipo moja kwa moja ni pamoja na RB Leipzig  atavaana na Atletico Madrid ambao waliwang’oa mabingwa watetezi Liverpool.
  Atalanta wabishi wa Serie A wao wataavana na  mabingwa wa Ligue 1 Paris Saint German ambapo katika hatua hiyo ya nusu fainali zitachezwa  mechi nne zikishirikisha timu nane.
 Michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itaanza kupigwa mwezi  ujao na itafanyika nchini Ureno katika jiji la Lisbon awali ilikuwa ifanyike Instanbul.
1.                 Madrid / Man City vs Lyon / Juventus
2.                 RB Leipzig vs Atletico Madrid
3.                 Napoli / Barcelona vs Chelsea /Bayern Munich
4.                 Atalanta vs Paris Saint-Germain
Kwa upande wa Europa League ambayo imefika  hatua ya robo fainali  kwa upande wake michezo ya hatua ya 16 mechi zake zote  hazikukamilika.
 Hivyo kwa Europa ratiba yao itakuwa hivi mshindi kati ya Shakhtar Donesk v Wolfburg atacheza na  Basel au Frankfurt, Man United v LASK mshindi atacheza na Copenhgen au Instanbul Basaksehir.
 Inter v Getafe  watacheza na mshindi kati ya Leverkusen au Rangers, huku mshindi kati ya Wolves v Olympiacos  atacheza na Roma au Sevilla na  fainali ya michuano hii itachezwa Ujerumani.
SOMA NA HII  MTUPIAJI NAMBA MOJA AZIINGIZA VITANI YANGA,AZAM NA SIMBA