Home Uncategorized KUHUSU SAKATA LA BERNARD MORRISON, UJUMBE WA JEMBE HUU HAPA

KUHUSU SAKATA LA BERNARD MORRISON, UJUMBE WA JEMBE HUU HAPA

 KWA sasa kinachoendelea kwenye masuala ya michezo ni sakata la kiungo mshambuliaji wa Yanga, Bernard Morrison ambaye ishu yake ipo kwenye Kamati ya Hadhi ya Wachezaji.


Kinacholeta mvutano ni suala la mkataba ambapo Morrison anasema kuwa alisaini dili la miezi sita huku Yanga ikieleza kuwa imempa kandarasi ya miaka miwili.

Pia Agosti 8 alitambulishwa ndani ya Simba huku habari zikieleza kuwa amesaini dili la miaka miwili.

Jana, Agosti 10 ilianza kuskilizwa kesi hiyo makao makuu ya Shrikisho la Soka Tanzania (TFF) na leo Agosti 11 inaendelea kuskilizwa huu hapa ujumbe wa Saleh Jembe:-Mpunguze presha leo mapema itajulikana, ushauri tuipe kamati muda majibu yapatikane lakini vizuri usiingizwe kwenye zile PROPAGANDA…


“Majibu yakitoka sote tunajua kabaki Yanga au kapitishwa Simba, maisha yanaendelea…

“Kawaida watu wa Kamati wanazima simu kabisa hadi wanapomaliza kikao.

“Zile sijui Hans Poppe kaondolewa, sijui Yanga wamebanwa ACHANA NAZO,” 


SOMA NA HII  FEDHA ZA EMMANUEL OKWI ZAIBULIWA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU, KAZI IPO