Home Uncategorized MWINYI ZAHERA AMALIZANA NA GWAMBINA KUANZA NA NYOTA HAWA KUTOKA YANGA

MWINYI ZAHERA AMALIZANA NA GWAMBINA KUANZA NA NYOTA HAWA KUTOKA YANGA

 MWINYI Zahera, ametambulishwa rasmi kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Gwambina FC ambayo imepanda daraja msimu huu wa 2019/20 na itashiriki Ligi Kuu Bara msimu wa 2010/21.

Zahera aliwahi kuifundisha Yanga ndani ya ligi msimu wa 2018/19 na alianza nayo msimu wa 2019/20 kabla ya kufungashiwa virago kwa kile kilichoelezwa kuwa aliboronga kwenye michuano ya kimataifa.

Kocha huyo amesaini dili la miaka mitano na inaelezwa kuwa ataanza kusajili nyota wake ambao alifanya nao kazi ndani ya Yanga.

Wanaotajwa kuibukia Gwambina ni pamoja na Mrisho Ngasa na Kelvin Yondani ambao kwa sasa ni wachezaji huru.

SOMA NA HII  LIVE:MAPOKEZI YA MABINGWA WA KOMBE LA MAPINDUZI YANGA BONGO