Home Uncategorized UONGOZI WA SIMBA WAZUNGUZUMZIA ISHU YA SENZO KUBWAGA MANYANGA

UONGOZI WA SIMBA WAZUNGUZUMZIA ISHU YA SENZO KUBWAGA MANYANGA


BAADA ya jana. Agosti 9 Senzo Mbatha aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Simba kutangaza kujiuzulu huku ikielezwa kuwa ameibukia kwa watani zao wa jadi Yanga, uongozi wa Simba umesema kuwa masiha lazima yaendelee.


Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara  amesema: “Ameondoka yeye lakini timu si inabaki kuendelea na maisha yake kwani ameondoka na timu? Simba ni kubwa kuliko mtu yoyote ameondoka hatumsemi vibaya shughuli zitaendelea hakuna jambo lolote ambalo linatutikisa.

“Simba ipo muda mrefu kabla ya Senzo, hata kama ameondoka bado Simba itazidi kuendelea kuwepo hakuna shabiki ambaye alitikisika hakuna kiongozi ambaye alitikisika,” amesema. 


Chanzo:Wasafi FM

SOMA NA HII  MECHI YA YANGA YAAHIRISHWA