Home Uncategorized BUNDESLIGA SASA MUBASHARA NDANI YA AZAM TV

BUNDESLIGA SASA MUBASHARA NDANI YA AZAM TV


MSIMU wa 2020/21 wa Ligi Kuu ya Ujerumani maarufu kama Bundesliga itarushwa moja kwa moja ndani ya chaneli ya  Azam TV.


Leo Septemba 15 umefanyika uzinduzi rasmi kwa ajili ya kuanza kurusha matangazo hayo ndani ya studi za Azam TV.

 Ligi hiyo ya Ujerumani itaonyeshwa katika kiwango cha HD kwa lugha ya Kiswahili kupitia kifurushi cha shilingi 18,000. Ligi hiyo inaanza Septemba 18, 2020.

Sasha Nella, Meneja wa Michezo wa Azam Media amesema kuwa:- “Hatutakuwa na La Liga, lakini tumeongeza nguvu kwenye Ligi Kuu Bara, (VPL) ili nayo ifikie viwango vya Bundesliga.” 

Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo imeanza kutimua vumbi Septemba 6 kwa sasa imeshakamilisha mzunguko wa pili na mechi zote 18 zimerushwa live ndani ya Azam TV.

SOMA NA HII  KIKOSI KAZI CHA POLISI TANZANIA LEO DHIDI YA YANGA, UWANJA WA USHIRIKA