Home Uncategorized KMC WAWEKA REKODI YA KIBABE VPL

KMC WAWEKA REKODI YA KIBABE VPL

 


WANA Kino Boys,  KMC ndio kikosi kilichoweka rekodi ya kufunga mabao mengi kuliko timu zote ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21.


Jumla kimepachika mabao 6 kibindoni kina pointi sita baada ya kucheza mechi mbili ambazo ni dakika 108 kwa msimu mpya ambao unaonekana kuwa na ushindani wa kipekee.


Safu yao ya ulinzi inayoongozwa na Andrew Vincent maarufu kama Dante imeruhusu bao moja ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons,  Uwanja wa Uhuru.


Kilianza kuwatungua Mbeya City, mabao 4-0 kikamaliza raundi ya pili kwa ushindi wa mabao 2-1 mbele ya Tanzania Prisons, zote Uwanja wa Uhuru.


Kinaongoza Ligi kwa sasa kikiwa na pointi sita huku Mbeya City ikiwa nafasi ya 18, 17 ni Coastal Union na 16 ni Mwadui FC zikiwa haziajaambulia pointi mechi mbili walizocheza.

SOMA NA HII  KLABU ZIWE ROHO YA MAKOCHA WAZALENDO LAKINI NAO…