Home Uncategorized CHELSEA YAKUBALI KUINASA SAINI YA KIPA WA RENNES

CHELSEA YAKUBALI KUINASA SAINI YA KIPA WA RENNES


CHELSEA imekubali kupata saini ya kipa wa Rennes, Edouard Mendy baada ya kufikia makubaliano ya kulipa pauni milioni 26 kama dau la kuipata saini yake.

Kipa huyo mwenye miaka 28 anatarajiwa kusaini dili la miaka mitano na awali dau lake lilikuwa linatajwa kuwa pauni milioni 22.

Kocha Mkuu wa Chelsea, Frank Lampard anahitaji kipa mpya ndani ya timu yake kwa ajili ya msimu huu wa 2020/21 ili kusaidiana na kipa namba moja ndani ya timu hiyo Kepa Arrizabalaga

Ikiwa dili la Mendy ambaye amecheza jumla ya mechi 34 kwenye timu yake litakamilika basi atafikisha idadi ya nyota saba ambao wamesaini ndani ya Chelsea.

SOMA NA HII  KOCHA SIMBA AJA KIVINGINE KABISA, ATAJA MALENGO TOFAUTI