Home Uncategorized SIMBA V BIASHARA UNITED KUKIWASHA LEO KWA MKAPA, REKODI HIZI ZINAONGEA

SIMBA V BIASHARA UNITED KUKIWASHA LEO KWA MKAPA, REKODI HIZI ZINAONGEA


LEO Septemba 20, Uwanja wa Mkapa, Simba itakuwa kazini majira ya saa 1:00 usiku ikimenyana na Biashara United mchezo wa Ligi Kuu Bara.


 Rekodi zinaonyesha kuwa timu hizi zimekutana mara nne ambapo Simba ilishinda mechi tatu na kupaa sare moja.


Biashara United haijaweza kupata pointi tatu mbele ya Simba hivyo leo itaingia uwanjani kupambana kuvunja rekodi hiyo.



Jumla ya mabao 10 yamepatikana kwa wapinzani hawa ambapo Simba imefunga mabao nane huku Biashara United ikifunga mabao mawili.


Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa wapo tayari kwa ushindani na wanahitaji pointi tatu na Kocha Mkuu wa Biashara United, Francis Baraza amesema kuwa wanahitaji pia pointi hizo.

Rekodi zao Simba v Biashara United zipo namna hii:-


2018/19
Biashara United 0-2 Simba.

Simba 1-1 Biashara United.

2019/20

Biashara 0-2 Simba.

Simba 3-1 Biashara United.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA