Home Uncategorized KAGERA SUGAR WAIWEKA KIPORO YANGA, SABABU IPO HIVI

KAGERA SUGAR WAIWEKA KIPORO YANGA, SABABU IPO HIVI

 


MECKY Mexime, Kocha Mkuu wa Kagera Sugar amesema kuwa wanaanza kumalizana kwanza na Gwambina Septemba 11 kisha Yanga itafuata Septemba 19.

Akizungumza na Saleh Jembe, Mexime amesema kuwa wanatambua ushindani ni mkubwa ndani ya Ligi Kuu Bara ila hesabu zao ni kuona wanafikia malengo waliyojiweka ya kupata pointi tatu.

“Mchezo wetu uliopita tumeachana nao sasa tunaipigia hesabu Gwambina, tupo vizuri na tukishamalizana na hawa Gwambina ndipo tutarudi Kaitaba kwa ajili ya kuanza kujiandaa dhidi ya Yanga,” amesema Mexime.

Kagera Sugar ilifungua pazia la ligi kwa kufungwa bao1-0 na JKT Tanzania, kwenye mchezo uliochezwa Septemba 7, Uwanja wa Kaitaba. 

Leo inamenyana na na Gwambina ambayo imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Biashara United, Uwanja wa Gwambina.

SOMA NA HII  KICHUYA ARUDI NA UTAMU WAKE