Home Uncategorized LAMPARD CHANZO CHA KAI HAVERTZ KUSAINI CHELSEA

LAMPARD CHANZO CHA KAI HAVERTZ KUSAINI CHELSEA

 

KAI Havertz, kiungo mpya ndani ya Klabu ya Chelsea amesema kuwa ushawishi wa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Frank Lampard ni sababu ya yeye kumwaga wino ndani ya timu hiyo.


Harvest amemwaga wino ndani ya Chelsea akitokea Klabu ya Bayer Leverkusen inayoshiriki Bundesliga kwa dau la thamani ya pauni 72 milioni.


Nyota huyo anatimiza idadi ya wachezaji sita ambao tayari wameshamalizana na Chelsea ikiwa ni pamoja na Timo Werner, Hakimi Ziyech,Malang Sarr,Thiago Silva na Ben Chilwell.


Amesaini dili la miaka mitano kutumika ndani ya Chelsea ambayo inashiriki Ligi Kuu England inayotarajiwa kuanza Septemba 12. 


“Maamuzi yangu ya kuja hapa Chelsea nilikuwa ninampenda Lampard na nilikuwa ninamfuatilia,”.

SOMA NA HII  SALAMBA AJIFUNGIA NDANI AKIPIGA MATIZI KULINDA KIPAJI CHAKE