Home Uncategorized NYOTA HAWA WATANO SIMBA KUIKOSA IHEFU FC LEO

NYOTA HAWA WATANO SIMBA KUIKOSA IHEFU FC LEO

 


LEO Septemba 6 Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza rasmi ambapo timu 12 zitakuwa uwanjani kusaka pointi tatu.


Mabingwa watetezi Simba nao pia watakuwa na kazi Uwanja wa Sokoine kumenyana na Ihefu FC ya Mbeya.

 Nyota wake watano wa kikosi cha kwanza wataukosa mchezo wa leo ikiwa ni pamoja na Pascal Wawa, Luis Miqussone, Chris Mugalu hawa wapo Dar es Salaam wakiendelea na mazoezi chini ya kocha wa viungo Adel Zraine.


Gerson Fraga kiungo mkabaji alikuwa na ruhusa maalumu kutokana na matatizo ya kifamilia.


Ibrahim Ame beki mpya ambaye alikuwa anakipiga ndani ya Coastal Union alipata majeraha kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya AFC Arusha hatma yake ipo mikononi mwa Sven Vandenbroeck kwa kuwa tayari ameanza mazoezi pamoja na timu kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba,Haji Manara.
SOMA NA HII  HASHEEM IBWE AWAOMBA WATANZANIA WAENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA