Home Uncategorized TRAORE AMALIZANA NA ASTON VILLA

TRAORE AMALIZANA NA ASTON VILLA


 ASTON Villa imethibitisha kukamilisha usajili wa Bertrand Traore kutoka Lyon. Traore hapo awali alikuwa akiichezea Ajax na Chelsea kabla ya kusaini Lyon misimu mitatu iliyopita.

Kocha Mkuu wa Aston Villa, Dean Smit amesema kuwa wanafurahi kumpata nyota huyo ndani ya kikosi hicho.

“Bertrand amechagua kuja Villa, ni mchezaji aliye na kipaji kikubwa ambaye atazidisha ubora kwenye safu ya ushambuliaji,” amesema.

Traore amesaini Villa kwa ada inayoripotiwa kuwa Euro mil. 18.4 ambayo inaweza kuongezeka kutokana na ubora wake ndani ya uwanja.

 Winga huyo mwenye umri wa miaka 25 alicheza mechi 126 kwenye mashindano yote na alifunga mabao 33 katika misimu mitatu.

SOMA NA HII  EVERTON YAIKOMALIA LIVERPOOL NA KUGAWANA POINTI MOJAMOJA KWENYE DABI