Home Uncategorized YANGA YATOA SHUKRANI KWA MASHABIKI WAKE

YANGA YATOA SHUKRANI KWA MASHABIKI WAKE


 UONGOZI wa Yanga umewashukuru mashabiki waliojitokeza kwa wingi jana kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Tanzania Prisons.


Mchezo huo ulichezwa Uwanja wa Mkapa na Yanga iligawana pointi mojamoja.


Bao la kwa Tanzania Prisons lilipachikwa kimiani na Lambart Sabiyanka na lile la kusawazishwa kwa Yanga lilipachikwa na Michael Sarpong.

Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio  Nugaz amesema kuwa mashabiki wanahitaji pongezi kwa kujitoa kuipa sapoti timu yao uwanja wa Mkapa.


“Mashabiki wengi walijitokeza katika hilo tunapenda kuwashuru na kusema asante kwa kujitokeza, ni mwanzo mzuri na imani yetu ni kwamba tutaendelea kujitokeza kwa wingi,” amesema. 

SOMA NA HII  ZANA KUSAINI MIAKA MIWILI SIMBA