Home Uncategorized PACHA YA CHIRWA NA DUBE INA MOTO KWELI

PACHA YA CHIRWA NA DUBE INA MOTO KWELI

 


PACHA ya nyota wawili ndani ya Klabu ya Azam FC imeweza kujibu ndani ya uwanja kutokana na kuwa na maelewano makubwa ndani ya uwanja.


Mpaka sasa wamefunga mabao 10 kwa pamoja kwenye Ligi Kuu Bara ndani ya Azam FC ambayo imefunga mabao 12.


Prince Dube amefunga mabao 6 na Obrey Chirwa amefunga mabao manne kwenye mechi ambazo wamecheza kwa msimu wa 2020/21.


Azam FC ikiwa imecheza mechi sita za ligi imeshinda zote na kuruhusu kufungwa mabao mawili ambapo kipa David Kissu amekusanya clean sheet tano.


Ushindi wa jana wa mabao 3-0 dhidi ya Mwadui umezidi kuwaweka nafasi ya kwanza wakiwa na pointi 18

SOMA NA HII  MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA UPO NAMNA HII