Home Uncategorized IHEFU YAJIPA MATUMAINI KUREJEA KWENYE UBORA

IHEFU YAJIPA MATUMAINI KUREJEA KWENYE UBORA

 


KOCHA Mkuu wa Ihefu FC, Zuber Katwila amesema kuwa wachezaji wake taratibu wanazidi kuimarika jambo ambalo linampa matumaini ya kufanya vizuri Kwenye mechi zake zijazo.


Ihefu FC imekuwa kwenye mwendo wa kusuasua msimu wa 2020/21 baada ya kupanda Ligi Kuu Bara kutoka Ligi Daraja la Kwanza iliposhinda kwa playoff dhidi ya Mbao FC.


Ipo nafasi ya 18 ikiwa imekusanya pointi 6 baada ya kucheza jumla ya mechi 11, mchezo wake wa raundi ya 11 ililazimisha sare ya bila kufungana na Polisi Tanzania,  Uwanja wa Azam Complex. 


Katwila amesema:”Bado kuna tatizo Kwenye upande wa umaliziaji wa nafasi ila kwa namna ambavyo tunakwenda taratibu tutakuwa imara,”.


Mchezo wake ujao itakuwa ni leo, Novemba 24 dhidi ya Coastal Union, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

SOMA NA HII  AZAM FC YAWAPNGA MKWARA MZITO FASIL KENEMA