Yanga SC

YANGA KUMSHUSHA MSHAMBULIAJI WAO MWILI JUMBA MUDA WOWOTE

admin January 26, 2021 9:47 am


 UONGOZI wa Yanga umesema kuwa nyota wao Michael Sarpong anatarajiwa kurejea muda wowote kuanza sasa baada ya kumaliza muda wake wa mapumziko.

Sarpong, wengi wanapenda kuwmita mwili jumba, ametupia mabao manne ndani ya Ligi Kuu Bara alitarajiwa kurejea jana kujiunga na kikosi kambini ila kuna mambo yalikwamisha mpango huo.

Meneja wa Klabu ya Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa nyota huyo atarejea muda wowote kuanza sasa.

“Tayari kikosi kimeanza mazoezi baada ya kuwasili kambini jana, Januari 25 hivyo bado kuna wachezaji ambao wanawasili kambini.

“Kuhusu Sarpong bado ni mchezaji wetu na anatarajiwa kurejea muda wowote kuanza sasa kwa kuwa alikuwa kwenye mapumziko, nchini Ghana,” amesema. 

ORODHA YA NYOTA 17 WA SIMBA AMBAO WAMEANZA KAZI NA MFARANSA HAWA HAPA NYOTA NANE HAWAJAANZA MAZOEZI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply