Home Uncategorized MZAMBIA WA SIMBA ASAINI KWA WAARABU

MZAMBIA WA SIMBA ASAINI KWA WAARABU


 MSHAMBULIAJI
Walter Bwalya aliyekuwa akikipiga ndani ya Klabu ya Nkana FC ya Zambia alipokuwa akicheza na Mtanzania Hassan Kessy amejiunga na Klabu ya Al Ahly ya Misri.


Nyota huyo mwenye rasta kichwani raia wa Zambia alikuwa anatajwa kuingia kwenye rada za mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ili kuongeza nguvu ndani ya kikosi hicho.


Baada ya kumalizana na Nkana, Bwalya aliibukia ndani ya El Gouna ila kwa ni mali ya Al Ahly Waarabu wa Misri akiwa amesaini kwa dili la miaka minne.


Nyota huyo mwenye miaka 25 anasifika kwa kujenga ushkaji na nyavu na kuwa na uzoefu wa soka la Afrika jambo ambalo limewavutia mabosi hao wa Misri.

SOMA NA HII  SHEVA: MUNGU AMETENDA MAAJABU NIPO KAMILI GADO