Home kimataifa HAALAD FITI KUANZA KAZI LEO MBELE YA SEVILLA

HAALAD FITI KUANZA KAZI LEO MBELE YA SEVILLA


 NYOTA wa Borrusia Dortumund, Erling Haalad anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachoanza leo dhidi ya Sevilla.

Nyota huyo licha ya kwamba anasumbuliwa na majeraha hivi karibuni anatajwa kuwa ndani ya kikosi hicho ndani ya uwanja.

Huu ni mchezo wa marudiano wa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambapo ni hatua ya 16 bora.

Haalad alipata madogo kwenye mchezo wa Bundesliga wikiendi iliyopita wakati timu yake ikisaka ushindi mbele ya Bayern Munich.

Kwenye mchezo huo dakika 90, ubao ulisoma Bayern Munich 4-2 Dortmund na aliweza kugongana na Boateng Jerome.

Kocha Mkuu wa Dortmund, Edin Terzic ameeleza kuwa nyota huyo yupo fiti kwa ajili ya mchezo dhidi ya Sevilla kwani amepona.

SOMA NA HII  PSG NYUMBANI KUWAVAA CITY LEO