Home epl ARSENAL YATAMBA KUREJEA KWENYE UBORA

ARSENAL YATAMBA KUREJEA KWENYE UBORA

 


NYOTA wa kikosi cha Arsenal,  Willian amesema kuwa anaamini uwepo wa Kocha Mkuu, Mikel Arteta utawarejesha kwenye ubora.


Winga huyo wa Arsenal,  raia wa Brazil amesema kuwa anaamini timu hiyo ipo mikono salama chini ya Arteta na itatamba kwa mara nyingine tena.


Ikumbukwe kwamba Arsenal haijashinda ubingwa wa Premier League tangu 2004 na kwa sasa haina uhakika wa kufanya hivyo.


Winga huyo amesema wapo kwenye mwendo mzuri chini ya msaidizi huyo wa zamani wa Pep Guardiola wa Manchester City. 


“Nadhani ina kila kitu cha kuifanya iwe na dira nzuri ni Klabu kubwa ipo mikono ya kocha bora ana kila kitu kitakachoifanya timu iwe bora,”.

SOMA NA HII  MBAPPE: KUHUSU MKATABA WANGU, SUBIRINI KWANZA