Home kimataifa CHELSEA YASEPA NA UEFA CHAMPIONS LEAGUE

CHELSEA YASEPA NA UEFA CHAMPIONS LEAGUE


BAO pekee la Kai Haverts wa Chelsea dakika ya 42 lilitosha kuipa timu hiyo ubingwa wa UEFA Champions League  mbele ya Manchester City ambao ni Mabingwa wa Ligi Kuu England. 

Mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Dragao majira ya saa 4:00 usiku ambapo mbinu za Kocha Mkuu wa Chelsea,  Thomas Tuchel zilimzidi Kocha Mkuu wa City, Pep Guardiola. 

Licha ya City kumiliki mpira asilimia 87 huku Chelsea wakiwa na asilimia 80 bado ngoma ilikuwa ni nzito kwao kuweka usawa na kushuhudia taji hilo likisepa na Chelsea.

SOMA NA HII  BRAZILI 'WAWEHUKA' NA TAARIFA ZA NEYMAR KUKOSEKANA MECHI ZOTE ZILIZOBAKI...