DROO ya Fainali ya Azam Sports Federation Cup inatarajiwa kufanyika kesho majira ya saa 5:00 asubuhi na itaruka mubashara Azam Sports1 HD.
Mabingwa watetezi wa taji hilo ni Simba na wametinga hatua ya robo fainali baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar, Uwanja wa Mkapa.
Hizi hapa ambazo zimetinga hatua ya robo fainali na zinasubiri kuona zitapangiwa na nani droo ya kesho:-
Rhino Rangers inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.
Biashara United, Azam FC, Mwadui FC, Yanga SC, Dodoma Jiji, Simba SC na Namungo FC.