Home kimataifa GRANIT BADO YUPOYUPO ARSENAL, ARTETA KASEMA

GRANIT BADO YUPOYUPO ARSENAL, ARTETA KASEMA


MIKEL Arteta, Kocha Mkuu wa Arsenal amesema kuwa mchezaji wake Granit Xhaka ataendelea kusalia ndani ya kikosi hicho.

Xhaka alikuwa anahusishwa kujiunga na AS Roma msimu ujao ambayo kwa sasa inanolewa na Kocha Mkuu, Jose Mourinho.

Kiungo huyo mkabaji kwa sasa amesaliwa na misimu miwili ndani ya Arsenal kwa kuwa mkataba wake utameguka msimu wa 2023.

Arteta amesema:”Granit ataendelea kuwa na sisi hapa kwani ni moja ya wachezaji muhimu kwetu,” . 

SOMA NA HII  PAMOJA NA KUITA WAGANGA WA KIENYEJI...MIKOSI YAZIDI KUMUANDAMA POGBA....