Home kimataifa KLOPP ATAJA KILICHOWAFANYA WAKAGAWANA POINTI MBELE YA BRENTFORD

KLOPP ATAJA KILICHOWAFANYA WAKAGAWANA POINTI MBELE YA BRENTFORD


JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool amesema kuwa wapinzani wao Brentford walistahili kupata pointi katika mchezo wao walipokutana kwenye Ligi Kuu England. 

Liverpool ililazimisha sare ya kufungana mabao 3-3 dhidi ya Brentford katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa juzi.

Klopp amesema kuwa timu yake ilicheza vizuri ila ilikutana na timu ambayo ilicheza vizuri sana.

“Timu yangu ilikwama kutokana na mipira mirefu iliyokuwa inapigwa na wapinzani lakini haina maana kwamba hatukufanya vizuri.

“Jambo pekee ambalo lilituangusha ni kuwania mipira iliyokufa jambo lililofanya tukapa matokeo haya na wapinzani wetu wanastahili kupata ambacho walikipata,” .

SOMA NA HII  NI WIKIENDI YA KIBABE YENYE MECHI KALI ZA KUBASHIRI NA MERIDIANBET....