Home news AHMED ALLY WA AZAM TV AKABIDHIWA ‘FUPA’ LA MANARA SIMBA…

AHMED ALLY WA AZAM TV AKABIDHIWA ‘FUPA’ LA MANARA SIMBA…


KLABU ya Simba imemtangaza Ahmed Ally kuwa Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, kabla ya kutangazwa kuwa Afisa Habari wa Simba, Ahmed Ally alikuwa mtangazaji wa Azam TV, lakini kabla ya hapo aliwahi kufanya kazi kwa muda mrefu kwenye kampuni ya Sahara Media [Radio Free Africa na Star TV].

Katika taarifa iliyotolewa na klabu ya Simba imemuelezea Ahmed kuwa ni kijana mchapakazi, mwenye uhusiano mzuri na watu wa aina zote, mtanashati na kubwa zaidi mwenye mapenzi yasiyopimika kwa klabu hiyo.

“Ni kijana mchapakazi, mwenye uhusiano mzuri na watu wa aina zote, mtanashati na kubwa zaidi mapenzi yake kwa Simba hayapimiki.

Ahmed Ally karibu kwenye klabu ya maisha yako kuwatumikia Wanasimba kama Afisa Habari na Mawasiliano”

SOMA NA HII  KISA SARE NA BIASHARA...KAMA KAWA KAZE HAKOSI SABABU...KAJA NA HII MPYA LEO...AWATUPIA MANENO SIMBA KUHUSIKA...