Klabu ya Namungo, kupitia mtendaji mkuu, Omary Kaaya, imeweka wazi kuwa, tetesi zinazosambaa juu ya Shiza Kichuya kuhusishwa kurejea Simba, wao haiwapi shida kwani wanachofahamu bado ni mchezaji wao.
Nyota huyo mara ya kwanza alijiunga na Simba Juni 2016 akitokea Mtibwa Sugar, akacheza hapo hadi Januari 2019, akatimkia Pharco ya Misri, kisha ENPPI, akarejea Simba Januari 2020.
Akizungmza, Kaaya alisema: “Shiza bado ni mchezaji wetu maana mkataba wake bado haujaisha, hivyo kama kweli Simba wanamuhitaji naamini muda wowote watakuja mezani ili tuone namna ya kumalizana nao.