Home Habari za michezo KOCHA SIMBA AWAONYESHA JEURI WYDAD CA…”HAWA MBONA FRESHI TU

KOCHA SIMBA AWAONYESHA JEURI WYDAD CA…”HAWA MBONA FRESHI TU

Habari za Simba leo

BAADA ya kupangwa na wanaotetea taji la Ligi ya Mabingwa Afrika, Wydad Casablanca ya Morocco katika mechi za robo fainali, kocha wa Simba, Roberto Oliveira ‘Robertinho’, amesema ; ‘Hawa mbona freshi tu’.

Mechi ya kwanza itachezwa Dar es SalaamAprili 21-22, kabla kurudiana wiki moja baadae, lakini Simba inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mara ya mwisho dhidi ya Wydad ndani ya dakika sita za mwisho.

Ikitinga nusu fainali itakutana na mshindi kati ya Mamelodi Sundowns ya Sauzi au CR Boulizdad ya Algeria.

Mashabiki kupitia mitandao ya kijamii wameonekana kupata ganzi kutokana na rekodi za timu za Morocco na wakikumbuka kipigo cha mabao 3-0 ilichopewa na wapinzani wao hao mwaka 2011, lakini kocha Robertinho amewatuliza na kuwaambia wamejipanga.

Kocha Robertinho aliliambia SOKA LA BONGO kuwa, kwa hatua hii waliyofikia hakuna timu nyepesi hivyo alitarajia kukutana na yoyote ili kuonyesha ukubwa wao na kwamba hata hao Wydad anaona ni sawa na watajipanga ili kuthibitisha kuwa hata Simba ni timu kubwa barani Afrika.

“Hakuna namna zaidi ya kupambana na aliyekuwa bora, tunakwenda kwenye hatua ngumu, hivyo tunahitaji kujiandaa vyema ila natambua hata wao pia wanahofia ubora wetu vilevile,”alisema na kuongeza kuwa ni ngumu kuwa bingwa bila kuwapiga mabingwa wenzio.

Robertinho ambaye ni kocha wa zamani wa Vipers alisema kitendo cha kuanzia nyumbani kutokana na kumaliza nafasi ya pili katika kundi kama ambavyo kanuni zinavyotaka hakiweza kuwaathiri, ushindi kokote.

Huu utakuwa ni mchezo wa sita kwa Simba kukutana na timu kutoka Morocco katika michuano ya Afrika.

Mei 28, 2011 ikutana na Wydad katika mchezo wa mchujo kuwania nafasi ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo katika mchezo huo ilipoteza kwa mabao 3-0, mechi iliyopigwa Uwanja wa Petro Sport uliopo huko jijini Cairo. Simba ilifungwa mabao hayo katika dakika sita za mwisho za mchezo huo.

Shirikisho la Soka Afrika liliamua timu hizo kukutana baaada ya Simba kushinda rufaa yake iliyoiwasilisha dhidi ya Mazembe ambayo ilimtumia kimakosa mchezaji wake, Besala Bokungu.

Mchezo wa pili kwa Simba kukutana na timu ya Morocco ulipigwa Februari 27 mwaka jana ambapo ilipoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya RS Berkane katika mechi ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika. Marudiano yalipochezwa Dar es Salaam Machi 13 mwaka jana ilishinda bao 1-0.

Msimu huu imekutana tena na timu ya Morocco, Raja Casablanca waliyokuwa kundi moja na kupasuka nje ndani kwa mabao matatu, ikichapwa 3-0 nyumbani kabla ya wikiendi iliyopita kulala tena 3-1 kwenye Uwanja wa Mohamed V, jijini Casablanca na sasa inarudishwa tena huko.

SOMA NA HII  HII HAPA MASHINE YA SIMBA YARUDI UWANJANI...NI BAADA YA KUKAA NJE MUDA MREFU